Tuesday, September 30, 2014

Wafanyakazi wa NBC waadhimisha Siku ya Moyo Duniani



Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) wakianza matembezi ya hisani ya takribani Kilomita 10 jijini Dar es Salaam ikiwa ni moja ya matukio ya benki hiyo kudhimisha Siku ya Moyo Duniani ambapo kiasi cha pesa watakachochangisha kitapelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kusaidia watoto na vijana wanaosumbuliwa na matatizo ya ugonjwa wa moyo. Siku ya Moyo Duniani huadhimishwa kimataifa Septemba 29 kila mwaka.

Baadhi ya wafanyakazi hao wakipita katika barabara ya Ocean Road kulekea maeoneo ya Coco Beach wakitokea makao makuu ya beni hiyo katika Tawi la Corporate, Posta Mpya.

Wafanyakazi hawa wa NBC wakiendelea na matembezi hayo ili kupata fedha kusaidia watoto na vijana wanaosumbuliwa na magonjwa ya moyo.


 Baada ya kumaliza matembezi hayo wafanyakazi hao wakipiga picha ya pamoja kuonyesha ushindi na mshikamano wao katika kusaidia watoto na vijana wanaosumbuliwa na matatizo ya magonjwa ya moyo.  

0 comments:

Post a Comment