Wednesday, March 18, 2015

Tanga Cement yatoa msaada kwa wahanga wa mafuriko Kahama.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Ally Rufuga (katikati) akipokea sehemu ya msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya sh milioni 17 kutoka kwa Meneja Biashara wa Kampuni ya Saruji Tanga (Tanga Cement Plc), Mattheus Roos vilivyotolewa  na kampuni hiyo kusaidia waathirika wa mvua ya mawe iliyotokea wilayani Kahama hivi karibuni. Hafla ya makabidhiano ilifanyika wilayani humo juzi. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya.

Meneja Mawasiliano ma Huduma za Jamii wa Tanga Cement Plc, B. Mtanga Noor (kushoto) akizungumza wakati wakikabidhi msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya sh milioni 17 kwa ajili ya wahanga wa mafuriko yaliyotokea wilayani Kahama hivi karibu. Hafla hiyo ilifanyika Kahama, Shinyanga juzi.  Kushoto kwake ni Meneja Biashara wa Tanga Cement, Mattheus Roos na Meneja Mauzo Taifa wa kampuni hiyo, Leslie Massawe na baadhi ya wafanyakazi wenzao.

0 comments:

Post a Comment