Wednesday, March 4, 2015

Benki ya Exim yakarabati kituo cha watoto wenye ulemavu Morogoro

Meneja wa Benki ya Exim Tawi la Morogoro, Bi Anna Wesiwasi (wapili kulia) akipeana mkono na Mkurugenzi wa Kituo cha Amani cha watoto wenye ulemavu, Padri Beatus Sewando (watatu kulia) mara tu baada ya kuzindua jengo la kituo hicho kilichokarabatiwa na benki hiyo jana mkoani Morogoro. Akishuhudia ni Afisa Mauzo wa Benki hiyo Vick Haji (Kulia). Picha na mpiga picha wetu.

BENKI ya Exim Tanzania imefanya ukarabati wa majengo ya kituo cha watoto wenye ulemavu cha Amani kilichopo eneo la Chamwino mkoani Morogoro ikiwa ni muendelezo wa jitihada za benki hiyo kuboresha maisha ya jamii.

Kupitia sera yake ya kurudisha sehemu ya faida yake kwa jamii, benki hiyo pia imejipanga kutoa misaada zaidi ikilenga mipango yenye kuleta maendeleo kwa jamii hapa nchini hususani katika maeneo ambayo benki hiyo tayari imefungua matawi yake.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya ukarabati wa majengo ya kituo hicho iliyofanyika mkoani humo mwishoni mwa wiki iliyopita, Meneja wa tawi la benki hiyo mkoani Morogoro, Bi Anna Wesiwasi alisema msaada huo pia unalenga uboreshaji wa maisha ya watoto wanaoishi kwenye kituo hicho kwa kuwa wataishi kwenye makazi salama, safi na bora kwa afya zao.

“Benki ya Exim siku zote tunaamini kuwa watoto wenye ulemavu wanahitaji kupewa matumaini zaidi na kwa kushiriki kwetu kwenye mipango ya maendeleo kama huu ndio tunatekeleza hiyo imani yetu kwa vitendo na zaidi tunazidi kuwa karibu na jamii inayotuzunguka jambo ambalo ni muhimu katika ulimwengu wa kibiashara kwa sasa kuona kwamba benki inarudisha sehemu ya faida yake kwa watu inao wahudumia,'' alisema Bi Wesiwasi

Kwa mujibu wa Bi Wesiwasi, benki hiyo inaamini kuwa watoto ndio wateja wao wa kesho kama sio wa sasa na hivyo basi benki hiyo itajitoa kwa hali na mali kuhakikisha kwamba wanapata maisha bora kwa sasa .

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo,  Mkurugenzi wa kituo hicho, Padri Beatus Sewando alisema uamuzi wa benki hiyo kusaidia kituo cha watoto wenye ulemavu ni kitendo kinachotakiwa kuigwa na taasisisi, mashirika na watu mbalimbali hapa nchini.

“Tunashukuru sana kuona wenzetu wa benki ya Exim wameonyesha mfano kwa kuitikia kilio chetu.Msaada huu utawahakikishia  watoto wetu hapa kituoni kuwa na makazi bora na salama kwaa afya zao…naomba wengione waige mfano huu,’’ alitoa wito

Related Posts:

  • MSD Imports Fake HIV Testing Kits FOUR people, including the Medical Stores Department (MSD) acting Director General, ignored expert advice and imported faulty HIV testing kits, subjecting the government to suffer an over two million US dollars (over … Read More
  • Donors now confirm withhold of Sh1tr aid Ms Sinikka Antila, Finnish ambassador and development  partners chairperson  It is now official. Development partners (DPs) have not released even a single dollar out of the $558 million (Sh937 billion), tha… Read More
  • Dar Rotary Marathon attracts 10,000 entries Bank M deputy CEO Jacqueline Woiso (C) speaking about the 2014 Rotary Dar Marathon. The marathon which is an annual event will be held on October 14. The Rotary Dar half Marathon 2014 hosted by the six clubs in Dar… Read More
  • Alcohol Abuse Fuelling Gender Violence, Survey Shows By Nelly Mtema MOST heavy drinkers start taking alcohol whey they are children, a baseline survey conducted by Tanzania Media Women's Association (TAMWA) on alcohol consumption and gender-based violence has revealed. … Read More
  • International Day of the Girl Child Empowering adolescent girls: Ending the cycle of violence  Message by UN Women Executive Director Phumzile Mlambo-Ngcuka on the occasion of the International Day of the Girl Child, 11 October 2014. On t… Read More

0 comments:

Post a Comment